Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 16 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..16...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu katika yote..

Yeye aliyetuamsha salama,Yeye atulindaye kila wakati,Yeye ni Mungu wetu na Muumba wetu,Yeye ni Baba yetu, Yeye ni Muweza wa yote,Yeye akisema ndiyo hakuna wakupinga,Yeye Ndimi Mwenyezi-Mungu..!!Yeye hubariki watu wake,,Yeye ni  mwenye huruma,Yeye husamehe,Yeye asifiwe,Yeye huponya,Yeye apokea maombi yetu,Yeye aokoa,Yeye asiye sinzia wala kulala,Mungu wetu yu mwema sana...


Hapo, Balaamu akamtolea Balaki kauli yake: “Inuka, Balaki, usikie, nisikilize ewe mwana wa Sipori. Mungu si mtu, aseme uongo, wala si binadamu, abadili nia yake! Je, ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize? Tazama, nimepewa amri ya kubariki, naye amebariki wala siwezi kuitangua. Mwenyezi-Mungu hajaona ubaya kwa wana wa Yakobo, wala udhia kwa hao wana wa Israeli. Mwenyezi-Mungu Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye husifiwa kwa vifijo miongoni mwao, yeye huzipokea sifa zao za kifalme. Mungu aliyewachukua kutoka Misri, huwapigania kwa nguvu kama za nyati. Hakika ulozi hauwezi kuwapinga watu wa Yakobo, wala uchawi dhidi ya watu wa Israeli. Sasa kuhusu Israeli, watu watasema, ‘Tazameni maajabu aliyotenda Mungu!’ Tazama! Waisraeli wameinuka kama simba jike, wanasimama kama simba dume. Ni kama simba asiyelala mpaka amalize mawindo yake, na kunywa damu ya mawindo.”
Mungu akatupiganie,Mungu akatutendee,Mungu akatulinde na kutuongoza,Mungu akatuokoe katika nguvu za giza,nguvu za mpinga Kristo zishindwe katika jina Kuu kushinda majina yote  la Bwana wetu Yesu Kristo,Mungu akatuinue na tukasimame imara..

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na Fadhili zako..

Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Mfalme wa Amani tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikoni mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe walio tukosea..
Utuokoe na mwovu na kazi zake zote,Ututakase Miili yetu na Akkili zetu kwa Damu ya mwanao Mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika maisha yetu tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..

Mungu wetu tunaomba utubariki na ukabariki vyote tunavyoenda kufanya/kutenda,kugusa/kutumia na ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Baba wa Mbinguni tunaomba ulinzi wako kwetu  sisi na vyote tunavyovimiliki vilivyo ndani na vilivyo nje Mungu wetu ukavifunike kwa Damu ya Bwana  wetu Yesu Kristo..
Mungu Baba ukaonekane kwenye maisha yetu na tusipungukiwe kwenye mahitaji yetu, popote tunapokuwa na chochote tunachofanya Mungu wetu ukajiinue na tukatende sawasaswa na mapenzi yako..
Tazama wenye shida/tabu,Yatima na Wajane,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokata tamaa,wenye hofu/mashaka,waliokataliwa/kutengwa pasipo sababu,waliokatika vifungo mbalimbali,wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukawaponye na kuwatendea sawasawa na mapenzi yako..

Sifa na utukufu ni kwako Mungu wetu..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako Mungu wetu..
Tuliyoyanena na tusiyoyanena Mungu wetu unayajua na kutujua vyema kuliko tujijuavyo wenyewe..

Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!
Asanteni sana wapendwa/waungwana kwa kuwa nami..
Mungu awe nanyi Daima..
sina neno zuri zaidi ya kusema..
Nawapenda.


Siku ya msamaha wa dhambi

1Mwenyezi-Mungu alizungumza na Mose, baada ya wana wawili wa Aroni kufa wakati ule walipomkaribia. 2#Taz Ebr 6:19 Alimwambia, “Mwambie ndugu yako Aroni asiingie mahali patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie mahali hapo kwani ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa. 3#Taz Ebr 9:7 Aroni ataingia mahali patakatifu sana akiwa na fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. 4Ataoga mwili wote katika maji, kisha atavaa mavazi matakatifu. Ataingia mahali hapo akiwa amevaa mavazi matakatifu: Joho la kitani baada ya nguo ya ndani ya suruali ya kitani na akiwa amevaa kanzu ya kitani na kujifunga mkanda wa kitani. 5Atatwaa kutoka jumuiya ya watu wa Israeli beberu wawili kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na kondoo dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
6“Aroni atamtoa huyo fahali sadaka ya kuondoa dhambi kwa ajili yake mwenyewe, na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na jamaa yake. 7Kisha, wale beberu wawili atawaweka kwenye mlango wa hema la mkutano. 8Atawapigia kura hao beberu wawili, kura moja kwa ajili ya Mwenyezi-Mungu na nyingine kwa ajili ya Azazeli. 9Atamleta yule beberu ambaye kura ilimtaka kwa ajili ya Mwenyezi-Mungu na kumtolea sadaka ya kuondoa dhambi. 10Lakini yule beberu aliyetakiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atatolewa mbele ya Mwenyezi-Mungu akiwa hai ili kufanya ibada ya upatanisho kuhani atamwacha aende jangwani kwa Azazeli, ili kuondoa dhambi za jumuiya.
11“Aroni atamtoa fahali wa sadaka ya kuondoa dhambi kwa ajili yake mwenyewe, na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya jamaa yake, kisha atamchinja fahali huyo sadaka ya kuondoa dhambi. 12Halafu atachukua chetezo na kutwaa makaa madhabahuni mbele ya Mwenyezi-Mungu na ubani konzi mbili uliosagwa vizuri sana. 13Ili asije akafa, atauleta ubani huo mbele ya Mwenyezi-Mungu na kuutia katika moto ili moshi wa ubani huo ukifunike kifuniko cha sanduku la agano. 14Atachukua kiasi cha damu ya yule fahali na kunyunyiza kwa kidole chake upande wa mashariki juu ya kiti cha rehema kisha atainyunyizia mbele ya sanduku la agano mara saba kwa kidole chake.
15 # Taz Ebr 9:12 “Halafu atamchinja yule beberu wa sadaka ya kuondoa dhambi kwa ajili ya watu wote. Damu ya mbuzi huyo ataileta ndani mahali patakatifu sana na kufanya kama alivyofanya na damu ya yule fahali; atainyunyiza juu ya kiti cha rehema, upande wake wa mbele. 16Hivyo atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya unajisi, makosa na dhambi zote za Waisraeli. Ndivyo atakavyofanya pia kwa ajili ya hema la mkutano lililo miongoni mwa watu hao walio najisi. 17Wakati Aroni anafanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, jamaa yake na jamii nzima ya Israeli, kamwe asiwepo mtu yeyote ndani ya hema la mkutano hadi atakapokuwa amemaliza na kutoka nje. 18Kisha atatoka na kwenda kwenye madhabahu iliyo mbele ya Mwenyezi-Mungu na kuifanyia ibada ya upatanisho. Atachukua kiasi cha damu ya yule fahali na ya yule mbuzi na kuzipaka pembe za madhabahu pande zote. 19Atainyunyizia madhabahu hiyo damu kwa kidole chake mara saba na hivyo kuiweka wakfu na kuitakasa unajisi wote wa watu wa Israeli.
20“Baada ya Aroni kumaliza kupatakasa mahali patakatifu, hema la mkutano na madhabahu, ndipo atamtoa yule beberu kwa ajili ya Azazeli,#16:20 Azazeli: Taz Lawi 16:8. akiwa hai. 21Aroni ataweka mikono yake juu ya kichwa cha huyo beberu hai na kuuungama juu yake dhambi zote za watu wa Israeli, makosa yao yote na dhambi zao zote, ili kumwajibisha huyo. Kisha atamwacha huyo beberu aende jangwani akipelekwa huko na mtu yeyote anayejitoa kwa hiari. 22Atamwacha huyo beberu aende jangwani, mahali pasipokuwa na watu, akiwa ameyachukua maovu yao yote.
23 # Taz Eze 44:19 “Kisha Aroni atarudi ndani ya hema la mkutano, atavua yale mavazi aliyovaa alipoingia mahali patakatifu sana na kuyaacha humo. 24Ataoga humo ndani katika mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake. Atatoka na kutoa sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka ya kuteketezwa ya watu wa Israeli, ili kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote. 25Mafuta ya sadaka ya kuondoa dhambi atayateketeza juu ya madhabahu. 26Yule mtu aliyempeleka yule beberu kwa Azazeli kwanza atayafua mavazi yake na kuoga ndipo atakapoweza kuingia kambini. 27#Taz Ebr 13:11 Yule fahali na mbuzi waliotolewa sadaka ya kuondoa dhambi ambao damu yao ilipelekwa mahali patakatifu sana ili kufanya ibada ya upatanisho, watapelekwa nje ya kambi na kuteketezwa. Ngozi zao, nyama na mavi yao, vyote vitateketezwa. 28Yule mtu atakayewateketeza atayafua mavazi yake na kuoga, ndipo atakapoweza kuingia kambini.
29 # Taz Lawi 23:26-32; Hes 29:7-11 “Hili ni sharti ambalo mnapaswa kulifuata milele: Siku ya kumi ya mwezi wa saba, nyinyi wenyewe na hata wageni wanaoishi miongoni mwenu, ni lazima mfunge siku hiyo na kuacha kufanya kazi. 30Mtafanya hivyo kwa sababu siku hiyo ndiyo siku ambayo mtafanyiwa ibada ya upatanisho, msafishwe dhambi zenu, nanyi mtakuwa safi mbele ya Mwenyezi-Mungu. 31Siku hiyo ni siku ya mapumziko kamili nanyi mtafunga. Kanuni hiyo ni ya kudumu milele. 32Kuhani aliyepakwa mafuta na kuwekwa wakfu ashike nafasi ya baba yake, ndiye atakayefanya ibada ya upatanisho akiwa amevaa mavazi matakatifu ya kitani. 33Atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu sana, kwa ajili ya hema la mkutano, madhabahu, makuhani na kwa ajili ya jumuiya nzima ya Israeli. 34Hili, basi ni sharti la kudumu milele; ni lazima mlifuate ili kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya watu wa Israeli mara moja kila mwaka na kusamehewa dhambi zao.” Mose akafanya yote kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.

Mambo Ya Walawi16;1-34


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 15 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..15...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Ni siku nyingine tena Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu,Muumba wa Vyote,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Yahweh..!Elohim..!El Shaddai,El Olam..!Jehova Nissi..!Jehovah Jireh..!Jehovah Rapha..!Jehovah Roi..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shalom..!
Muweza wa yote,Hakuna kama wewe Baba..!!
Asante Mungu wetu kwa wema na Fadhili zako..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote...
Asante kwa kutuamsha tena na kutuchagu,Umetupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tunakushuru Mungu wetu  katika yote wewe ni wakuabudiwa Daima..
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Jehovah..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizoziwaza,tulizonena,tulizotenda,tunazozijua/tusizozijua..

Mungu wetu tunaomba nasi ukatupe neema ya kuweza kuwasamehe wale walio tukosea..
Ukatuepushe na majaribu yote Mungu wetu,Ukatuokoe na yule mwovu na kazi zake zote,Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu na ukatufunike na Damu ya Mwanao Mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..
Baba wa Mbinguni ukatamalaki na kutuatamia  katika nyumba zetu/maisha yetu, Ndoa zetu Baba wa Mbinguni tunaziweka mikononi mwako,Ukatuongoze vyema na kila mmoja akajue wajibu wake,Wanawake ukatupe neema ya Kutii na Wanaume ukawaongoze katika mapenzi yao kwetu,Ukatuepushe na mifarakano isiyo na faida,ukatupe kutambua Amri na Sheria zako..

Ukawafunike kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo na ukawalinde na kuwaokoa watoto wetu na hatari zote,ukawaongoze vyema na hatua zao ziwe nawe Baba wa Mbinguni,kwenye masomo yao Baba ukawape ufahamu,Uelewa na kumbukumbu kwa yote waliyofundishwa,kwenye michezo na maisha yao yapo juu yako Mungu wetu..
Ukatupe Hekima,Busara katika malezi yetu,ukatuongoze Mungu wetu na tukawe wazazi/walezi wema na wenye kuwafundisha yaliyo yako.



Maisha ya kale na maisha mapya

Enyi wake, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana. Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao. Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana. Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa. Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana. Kila mfanyacho, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu. Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana! Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
Tunakushukuru ee Mungu wetu na tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!
Asanteni sana Wapendwa kwakunitembela/kunisoma..
Mungu akawaongoze katika yote..
Nawapenda.

Vitu najisi vya mwili

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose na Aroni, 2“Waambieni Waisraeli hivi: Mwanamume yeyote akitokwa na usaha, usaha huo wamfanya kuwa najisi. 3Na ufuatao ni mwongozo kuhusu najisi hiyo: Muda wote anapotokwa na usaha au usaha unapokuwa umezuiwa ndani yake, mtu huyo ni najisi. 4Kitanda chochote atakacholalia au atakachokalia, kitakuwa najisi. 5Mtu yeyote atakayegusa kitanda chake mtu huyo ni lazima ayafue mavazi yake, na kuoga; naye atakuwa najisi mpaka jioni. 6Mtu yeyote atakayekalia kitu chochote alichokalia huyo mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima ayafue mavazi na kuoga; na atakuwa najisi hadi jioni. 7Mtu yeyote atakayemgusa mtu atokwaye na usaha, lazima afue mavazi yake na kuoga; naye atakuwa najisi mpaka jioni. 8Mtu yeyote akitemewa mate na mtu anayetokwa usaha ni lazima mtu huyo aliyetemewa mate ayafue mavazi yake, na kuoga; naye atakuwa najisi mpaka jioni. 9Tandiko lolote la mnyama aliloketia mtu anayetokwa na usaha litakuwa najisi. 10Mtu yeyote atakayegusa kitu chochote alichokalia mtu huyo, atakuwa najisi mpaka jioni. Mtu yeyote anayebeba kitu chochote kilichokuwa cha mtu huyo ni lazima ayafue mavazi yake, na kuoga; naye atakuwa najisi mpaka jioni. 11Mtu yeyote anayetokwa na usaha akimgusa mtu bila kusafisha kwanza mikono yake na kuoga, aliyeguswa atakuwa najisi mpaka jioni. 12Chombo chochote cha udongo kilichoguswa na mtu anayetokwa na usaha ni lazima kivunjwe. Lakini chombo chochote cha mbao ni lazima kisafishwe kwa maji.
13“Mwanamume yeyote anayetokwa na usaha akiponywa ugonjwa wake, ni lazima huyo mtu angoje siku saba kabla ya kuondolewa unajisi wake. Atayafua mavazi yake na kuoga kwa maji ya mtoni; naye atakuwa safi. 14Siku ya nane, ni lazima alete hua wawili au makinda mawili ya njiwa mbele ya Mwenyezi-Mungu mlangoni mwa hema la mkutano na kumkabidhi kuhani. 15Kuhani atawatoa hao, mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; naye kuhani atamfanyia huyo mtu ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu na kumwondolea unajisi wake wa kutokwa na usaha.
16“Kama mwanamume yeyote akitokwa na shahawa yake, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 17Vazi lolote lililodondokewa shahawa au ngozi yoyote iliyoguswa na shahawa hiyo ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni. 18Kama mwanamume akilala na mwanamke, akatokwa na shahawa, basi, ni lazima wote wawili waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.
19“Mwanamke yeyote anapokuwa mwezini, atakuwa najisi kwa muda wa siku saba. Mtu yeyote atakayemgusa mwanamke huyo atakuwa najisi mpaka jioni. 20Kitu chochote anacholalia au kukalia wakati yu najisi, kitakuwa najisi. 21Mtu yeyote atakayegusa kitanda cha huyo mwanamke ni lazima ayafue mavazi yake na kuoga kwa maji; naye atakuwa najisi mpaka jioni. 22Mtu yeyote atakayegusa kitu chochote anachokalia mwanamke huyo ni lazima ayafue mavazi yake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 23Mwanamume yeyote atakayegusa kitu chochote alicholalia au kukalia huyo mwanamke, atakuwa najisi mpaka jioni. 24Kama mwanamume akilala na mwanamke huyo na damu ya huyo mwanamke ikamdondokea huyo mwanamume, basi, mwanamume huyo atakuwa najisi kwa muda wa siku saba. Kitanda chochote atakacholalia huyo mwanamume kitakuwa najisi.
25“Kama mwanamke anatokwa na damu kwa muda wa siku nyingi kuliko ilivyo kawaida au anatokwa damu wakati usio wa majira yake ya kutokwa damu, basi, ataendelea kuwa najisi muda wote damu inapomtoka. 26Kitanda chochote anacholalia wakati huo au kiti chochote anachokalia, kitakuwa najisi sawa kama wakati wa unajisi wake wa kutokwa damu. 27Mtu yeyote atakayegusa vitu hivyo, atakuwa najisi na ni lazima ayafue mavazi yake na kuoga; naye atakuwa najisi mpaka jioni. 28Baada ya kukauka damu yake mwanamke huyo atangoja hadi siku saba ili kuwa safi; na baada ya muda huo atakuwa safi. 29Siku ya nane atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa na kumletea kuhani mlangoni mwa hema la mkutano. 30Kuhani atamtoa mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Hivyo kuhani atamfanyia huyo mwanamke ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu na kumwondolea unajisi wake wa kutokwa damu.
31“Ndivyo mtakavyowatahadharisha Waisraeli na unajisi wao, wasije wakaikufuru maskani yangu takatifu iliyo miongoni mwao wakiingia humo na unajisi wao; wakifanya hivyo watauawa.”
32Hiyo ndiyo sheria kuhusu mwanamume anayetokwa na usaha na anayetokwa na shahawa na kuwa najisi. 33Sheria hiyo yamhusu pia mwanamke anayetokwa damu na kuwa najisi. Sheria hiyo yamhusu mwanamume au mwanamke yeyote anayetokwa na chochote na pia yahusu mwanamume anayelala na mwanamke ambaye ni najisi.

Mambo Ya Walawi15;1-33


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 14 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..14...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Mungu wetu,Baba yetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo ni mali yako,Hata sisi ni mali yako Baba,Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo..
Asante kwa wema na fadhili zako Mungu wetu..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote Yahweh..!
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii Mngu wetu..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Muumba wetu..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..

Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Baba wa Mbinguni utuepushe na majaribu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu na utufunike kwa Damu ya Mwanao Mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti .
Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukapate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..
Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako tunaomba utubariki na kubariki kazi zetu,Biashara,Masomo,tuingiapo/tutokapo,vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahaweh..
Ukabariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Tazama wenye shida/tabu, wanapoitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokatika vifungo mbalimbali Mungu wetu ukawaguse na mkono wako wenye nguvu ukawaponye na kuwaokoa katika mapito yao..


Wapendwa/Waungwana; Mungu akatupe Kibali Leo na wakati mwingine cha kuwaombea Ndugu/jamaa zetu na watu wengine..

Jehovah tunaweka nyumba zetu,familia,ndugu,jamaa na wote wanaotufahamu kwa namna moja au nyingine na wote wanaosoma hapa..

Baba wa Mbingu tunaomba ukatulinde na kutuokoa,ukatuponye kiroho na ukatupe amani ya moyo, ukatujenge kiroho/kiimani,tukaijue kweli yako na kukufuata wewe Mungu na kufuata sheria zako,Agano lako na Amri zako..Ukatufadhili ee Mungu wetu na kutuhurumia,Ukatusamehe na ukatuepushe na Hasira,Chuki,Wivu,Tamaa,Masimango,Kujisifu/kujikweza, kisasi na yote yasiyo kupendeza wewe..
Ee Mungu wetu ukatuinue na kutusimamisha, tazama ndugu zetu walio asi Mungu wakurudie pasipo na aibu wakapate Nuru na Mwanga kwenye maisha yao...

Lifuatalo ni simulizi la Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa, nilipokuwa katika mji mkuu wa Susa, katika mwezi wa Kislevu wa mwaka wa ishirini, Hanani, mmoja wa ndugu zangu, akaja pamoja na baadhi ya watu toka nchini Yuda. Nikawauliza kuhusu Wayahudi wenzetu waliosalimika, yaani ambao hawakuhamishiwa Babuloni na kuhusu mji wa Yerusalemu. Wao wakaniambia, “Wayahudi waliosalimika na kubaki katika mkoa ule, wako katika taabu na aibu. Ukuta wa mji wa Yerusalemu umebomolewa na malango yake yameteketea.” Niliposikia hayo nilikaa chini na kulia, nikaomboleza kwa siku kadhaa. Nikafunga na kumwomba Mungu wa mbinguni, nikisema, “Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa mbinguni, wewe u Mungu aliye mkuu na wa kutisha, unalishika agano lako na unawafadhili wale wakupendao na kuzishika amri zako. Yasikilize kwa makini maombi yangu, na uniangalie mimi mtumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na mchana. Ninaungama dhambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya dhambi. Tumetenda mabaya mbele yako, hatujazishika amri zako, kanuni na maagizo yako uliyomwagiza mtumishi wako Mose. Kumbuka sasa lile ulilomwambia mtumishi wako Mose, uliposema, ‘Kama hamtakuwa waaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa. Lakini mkinirudia, mkazishika amri zangu na kuzifuata hata ingawa nitakuwa nimewatawanya mbali kabisa, nitawarudisha mahali nilipochagua kuwa mahali pangu pa kuabudiwa.’ Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mkono wako wenye nguvu. Ee Bwana, yasikie maombi yangu mimi mtumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Nakuomba unifanikishe leo, mimi mtumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mfalme.” Basi, mimi nilikuwa na jukumu la kumpa mfalme kinywaji.
Mungu wetu tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako
ee Mungu wetu na ukasikie kulia kwetu na kupokea maombi/sala zetu..
Asante Mungu wetu na tunayaweka haya yote mikononi mwako...
Tunakushukuru na kukusifu Daima..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Asanteni sana kwakunisoma/kutembelea hapa..
Mbarikiwe na Ninawapenda.



Utakaso baada ya kuugua magonjwa ya ngozi

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Ifuatayo ni sheria kumhusu mwenye ukoma katika siku ya kutakaswa kwake. Baada ya kupona ataletwa kwa kuhani. 3Kuhani atakwenda kumwangalia huyo mtu nje ya kambi. Ikiwa ukoma huo umepona, 4basi, kuhani ataamuru watu walete ndege wawili safi walio hai, kipande cha mwerezi, sufu ya rangi nyekundu na tawi la husopo kwa ajili ya huyo mtu atakayetakaswa. 5Kuhani atawaamuru wamchinje ndege mmoja katika chungu chenye maji safi ya chemchemi. 6Kuhani atamchukua yule ndege mwingine hai, kipande kile cha mwerezi, sufu ya rangi nyekundu na lile tawi la husopo na kuvitumbukiza vyote katika damu ya yule ndege aliyechinjwa. 7Kisha, atamnyunyizia huyo mwenye kutakaswa ile damu mara saba, halafu atamtangaza mtu huyo kuwa safi. Yule ndege hai atamwacha aende zake mashambani nje ya mji. 8Huyo mtu atayafua mavazi yake, atanyoa nywele zake, na kuoga; naye atakuwa safi. Baada ya hayo atarudi kambini, lakini atakaa nje ya hema lake kwa muda wa siku saba. 9Siku ya saba atanyoa nywele zake zote, ndevu na kope za macho yake. Kisha atafua mavazi yake na kuoga, ataoga kwa maji; naye atakuwa safi.
10“Siku ya nane ataleta wanakondoo madume wawili wasio na dosari, kondoo jike wa mwaka mmoja asiye na dosari, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka pamoja na mafuta theluthi moja ya lita. 11Kuhani atakayemtakasa mtu huyo atamleta mbele ya Mwenyezi-Mungu karibu na mlango wa hema la mkutano pamoja na vitu alivyoleta. 12Kuhani atachukua mwanakondoo dume mmoja na kumtolea sadaka ya kuondoa hatia pamoja na yale mafuta theluthi moja ya lita. Atafanya ishara ya kuvitolea mbele ya Mwenyezi-Mungu. 13Kisha atamchinja huyo mwanakondoo katika mahali patakatifu, wanapochinjia wanyama wa sadaka ya kuondoa dhambi na sadaka ya kuteketezwa. Sadaka hii ya kuondoa hatia, kama ilivyo sadaka ya kuondoa dhambi, ni mali yake kuhani; ni sadaka takatifu kabisa. 14Kuhani atachukua kiasi cha damu ya sadaka ya kuondoa hatia na kumpaka mtu anayetakaswa katika ncha ya sikio lake la kulia na kidole gumba cha mkono wake wa kulia na kidole gumba cha mguu wake wa kulia. 15Kisha, kuhani atachukua kiasi cha ile theluthi moja ya mafuta na kuyatia katika kiganja cha mkono wake wa kushoto. 16Atachovya kidole cha mkono wake wa kulia katika mafuta hayo na kumnyunyizia huyo mtu anayetakaswa mara saba mbele ya Mwenyezi-Mungu. 17Kiasi cha mafuta yanayobaki katika kiganja chake atampaka huyo mtu anayetakaswa katika ncha ya sikio lake la kulia na kidole gumba cha mkono wake wa kulia na kidole gumba cha mguu wake wa kulia, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia. 18Yale mafuta yaliyobaki atampaka huyo mtu kichwani. Hivyo kuhani atamfanyia ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu. 19Kuhani atatolea sadaka ya kuondoa dhambi na kumfanyia huyo mtu anayetakaswa ibada ya upatanisho ili kumwondolea unajisi wake. Kisha atamchinja mwanakondoo wa sadaka ya kuteketezwa. 20Kuhani atatolea ile sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka juu ya madhabahu. Hivyo kuhani atamfanyia huyo mtu ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.
21“Lakini ikiwa mtu huyo ni maskini, hana uwezo wa kutoa vitu hivyo, basi ataleta mwanakondoo dume mmoja kuwa fidia ya sadaka ya kuondoa hatia ambaye atafanyiwa ishara ya kutoa sadaka ili kumfanyia huyo mtu ibada ya upatanisho. Ataleta pia kilo moja ya unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka na mafuta theluthi moja ya lita. 22Ataleta pia hua wawili au makinda mawili ya njiwa kadiri anavyoweza mmoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. 23Siku ya nane atamletea kuhani vitu hivyo mbele ya mlango wa hema la mkutano kwa ajili ya utakaso wake mbele ya Mwenyezi-Mungu. 24Kuhani atamchukua huyo mwanakondoo dume wa sadaka ya kuondoa hatia pamoja na yale mafuta theluthi moja ya lita na kufanya ishara ya kuvitolea mbele ya Mwenyezi-Mungu. 25Atamchinja huyo mwanakondoo dume wa sadaka ya kuondoa hatia. Kuhani atachukua kiasi cha damu na kumpaka huyo mtu anayetakaswa katika ncha ya sikio lake la kulia, katika kidole gumba cha mkono wake wa kulia na kidole gumba cha mguu wake wa kulia. 26Kuhani atatia kiasi cha mafuta hayo katika kiganja cha mkono wake wa kushoto. 27Kisha atamnyunyizia huyo mtu kwa kidole chake cha kulia kiasi cha hayo mafuta yaliyomo katika kiganja chake cha kushoto mara saba mbele ya Mwenyezi-Mungu. 28Kuhani atampaka huyo mtu anayetakaswa mafuta katika ncha ya sikio lake la kulia, katika kidole gumba cha mkono wake wa kulia, na kidole gumba cha mguu wake wa kulia. Atampaka mahali pale ambapo alimpaka ile damu ya sadaka ya kuondoa hatia. 29Mafuta yanayosalia mkononi mwake atampaka huyo mtu kichwani, ili kumfanyia ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu. 30Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale hua au njiwa wawili kadiri mtu huyo anavyoweza kuleta. 31Hua atakuwa kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Pamoja na hao, atatoa sadaka ya nafaka; naye kuhani atamfanyia huyo mtu ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu. 32Huo ndio mwongozo kuhusu mtu mwenye ukoma asiyeweza kutoa sadaka za kumtakasa.”

Upele katika nyumba

33Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose na Aroni, 34“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikafanya namna ya upele wa ukoma uote katika ukuta wa nyumba fulani katika nchi mtakayoimiliki, 35basi, mwenye nyumba hiyo ni lazima amwambie kuhani kwamba namna ya upele wa ukoma umeonekana katika nyumba yake. 36Kuhani ataamuru vitu vyote ndani ya nyumba hiyo vitolewe kabla yeye mwenyewe hajaanza uchunguzi wake; visije vyote kutangazwa kuwa najisi. Kisha kuhani ataingia kuiangalia nyumba hiyo. 37Atauchunguza upele huo; kama upele huo umeonekana ukutani na umesababisha madoa ya rangi ya kijani kibichi au nyekundu na kuonekana kuwa yamepenya ndani ya kuta, 38basi, kuhani atatoka nje mlangoni na kuifunga nyumba hiyo kwa muda wa siku saba. 39Siku ya saba kuhani atarudi na kuiangalia tena nyumba hiyo. Ikiwa upele huo umeenea katika kuta za nyumba hiyo, 40kuhani ataamuru mawe yaliyoko kwenye sehemu zenye upele yatolewe na kutupwa mahali najisi nje ya mji. 41Lipu ya nyumba hiyo itabanduliwa na kifusi chake kutupwa mahali najisi nje ya mji. 42Kisha watachukua mawe mapya na kujenga mahali walipobomoa; nao wataipiga nyumba hiyo lipu upya.
43“Ikiwa upele huo utatokea tena baada ya kutoa mawe hayo na kukwangua lipu na kuipiga lipu upya, 44yapasa kuhani aje kuichunguza. Ikiwa upele umeenea katika nyumba hiyo, basi huo ni upele wa kufisha; nyumba hiyo ni najisi. 45Nyumba hiyo ni lazima ibomolewe na mawe yake, miti yake na lipu vipelekwe mahali najisi nje ya mji. 46Zaidi ya hayo, yeyote atakayeingia ndani ya nyumba hiyo wakati itakapokuwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni. 47Yeyote anayelala katika nyumba hiyo au kulia chakula ndani yake, lazima ayafue mavazi yake.
48“Lakini ikiwa baada ya kuikagua nyumba hiyo, kuhani ataona kuwa upele haujaenea baada ya kupigwa lipu, basi, kuhani atatangaza kuwa nyumba hiyo ni safi kwani upele umekwisha. 49Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili pamoja na kipande cha mwerezi, sufu nyekundu na tawi la husopo. 50Atamchinja ndege mmoja katika chungu chenye maji safi ya chemchemi. 51Atachukua kipande cha mwerezi, tawi la husopo na ile sufu nyekundu pamoja na yule ndege mwingine aliye hai na kuvitumbukiza vyote katika damu ya yule ndege aliyechinjwa. Kisha atainyunyizia nyumba hiyo damu mara saba. 52Hivyo ndivyo atakavyoitakasa nyumba hiyo kwa damu ya ndege, maji safi ya chemchemi, ndege hai, kipande cha mwerezi, tawi la husopo na ile sufu nyekundu. 53Yule ndege hai atamwacha aende zake mashambani nje ya mji. Hivyo ndivyo atakavyoitakasa nyumba hiyo, nayo itakuwa safi.”
54Hii ndiyo sheria kuhusu aina yoyote ya namna ya upele wa ukoma; 55upele katika nguo au nyumba, 56uvimbe, jipu au kipaku, 57ili kuonesha ni kitu gani kilicho najisi na kisicho najisi. Hiyo ndiyo sheria kuhusu namna ya upele wa ukoma.

Mambo Ya Walawi14;1-57


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 13 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..13...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Ni siku nyingine tena Mungu ametuchagua na  ametupa Kibali cha kuendelea kuiona siku hii...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako..

Asante kwa ulinzi wako usiku na wakati wote..
Asante kwakutuamsha salama na wenye Afya..

Tunashukuru na kukusifu Daima..
Tunashuka mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..

Utuepushe katika majaribu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo..yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote,Tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..

Ukatubariki na kubariki vyote tunavyoenda kufanya/kutenda...

kuingiakwetu/kutoka kwetu na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Mfalme wa Amani ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..

Tazama wenye shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu,waliokatika vifungo mbalimbali.. Baba wa mbinguni nyoosha mkono wako wenye nguvu ,ukawaokoe katika mapito yao na ukawaponye kimwili na kiroho pia,ukawajibu na kuwafuta machozi wote wanaokuomba na kukukimbilia..Mungu ukaonekane kwenye mahitaji yao..
Na ukawape sawasawa na mapenzi yako..

Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia..
tukatii na kufuata Neno lako..
Tukaishi kwa kukutegemea wewe zaidi..
ukatupe maarifa na ubunifu katika kazi zetu,Biashara zetu..
popote tupitapo ukaonekane Mungu wetu..
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako...


Bwana Mungu amenipa ufasaha wa lugha, niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubuhi hunipa hamu ya kusikiliza anayotaka kunifunza. Bwana Mungu amenifanya msikivu, nami sikuwa mkaidi wala kugeuka mbali naye. Mgongo wangu niliwaachia walionipiga, mashavu yangu waliozingoa ndevu zangu; walioniaibisha na kunitemea mate, sikujificha mbali nao. Bwana Mungu hunisaidia, kwa hiyo siwezi kufadhaika. Uso wangu nimeukaza kama jiwe; najua kwamba sitaaibishwa. Mtetezi wangu yuko karibu. Ni nani atakayepingana nami? Na aje tusimame mahakamani. Adui yangu ni nani? Na ajitokeze mbele basi. Tazama Bwana Mungu hunisaidia. Ni nani awezaye kusema nina hatia? Maadui zangu wote watachakaa kama vazi, nondo watawatafuna. Nani kati yenu amchaye Mwenyezi-Mungu? Nani anayetii maneno ya mtumishi wake? Kama yupo atembeaye gizani bila taa, amtumainie Mwenyezi-Mungu, na kumtegemea Mungu wake. Lakini nyinyi mnaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, tembeeni kwa mwanga wa moto huo, miali ya moto mliowasha nyinyi wenyewe. Mtakachopata kutoka kwa Mwenyezi-Mungu ni hiki: Nyinyi mtalala chini na mateso makali.


Tunakutumainia wewe siku zote na kukusifu Daima..
Tunakushukuru katika yote na kukutukuza Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote mimkononi mwako Mungu wetu..
Tukiamini wewe ni Mungu wetu na hatuna Mungu mwingine..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Niwashukuru sana wote mnaondelea kupita hapa..
Mungu akaonekane kwenye maisha yenu..
msipungukiwe katika mahitaji yenu na akawape sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda.

Sheria kuhusu ukoma

1Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, 2“Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au kipaku mwilini mwake, ikadhihirika kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Aroni au mmoja wa wanawe aliye kuhani. 3Kuhani atapakagua mahali palipo na ugonjwa na ikiwa nywele za mahali hapo zimebadilika kuwa nyeupe na ugonjwa wenyewe ukionekana kuwa uko ndani zaidi ya ngozi ya mwili wake, basi, huo ni ukoma. Kuhani akimaliza kumkagua, hivyo atatangaza kuwa mtu huyo ni najisi. 4Lakini ikiwa kipele hicho, ingawa cheupe hakikuingia ndani sana ya ngozi na wala nywele za mahali hapo hazikubadilika kuwa nyeupe, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda wa siku saba. 5Siku ya saba, kuhani atamwangalia tena mtu huyo, na ikiwa, kulingana na uchunguzi wa kuhani, ugonjwa huo haujaenea kwenye ngozi yake, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku nyingine saba.
6“Kuhani atamkagua tena mtu huyo siku ya saba. Kama kulingana na uchunguzi wake, ile sehemu ya ugonjwa imefifia na ugonjwa haujaenea, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi; huo ni upele tu. Mtu huyo atafua mavazi yake, naye atakuwa safi. 7Lakini upele huo ukiwa umeenea kwenye ngozi, baada ya mtu huyo kujionesha kwa kuhani kwa ajili ya kutakaswa kwake, basi, atakuja tena kwa kuhani. 8Kuhani atamwangalia tena, na kama ule upele umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; huo ni ukoma.
9“Kama mtu ameshikwa na ukoma, ataletwa kwa kuhani. 10Kuhani atamwangalia na kama kuna uvimbe mweupe ambao umezifanya nywele zake ziwe nyeupe na uvimbe huo umegeuka kuwa kidonda kibichi, 11huo ni ukoma wa muda mrefu. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hakuna haja ya kumweka mtu huyo kwa uchunguzi kwani yu najisi tayari. 12Kama ukoma umemshika na umeenea mwili mzima, toka utosini hadi nyayoni kama atakavyoona kuhani, 13hapo kuhani atamwangalia. Kuhani akiona kuwa ukoma umemwenea mwili mzima, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa safi kwa sababu mwili umegeuka kuwa mweupe na hivyo mtu huyo yu safi. 14Lakini kukionekana mwilini mwa mtu huyo kidonda kibichi, basi, mtu huyo atakuwa najisi. 15Kuhani ataangalia hicho kidonda kibichi na kumtangaza kuwa ni najisi kwa sababu huo ni ukoma. 16Lakini hicho kidonda kikigeuka tena kuwa cheupe, mtu huyo atarudi kwa kuhani. 17Kuhani atamwangalia na akiona kuwa kimegeuka kuwa cheupe, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa safi.
18“Kama mtu ameshikwa na jipu, nalo limepona, 19lakini mahali pale lilipokuwa jipu pamegeuka kuwa uvimbe mweupe au kuwa pekundu lakini peupe kiasi, ni lazima kumwonesha kuhani. 20Kuhani atamwangalia huyo mtu. Kuhani akiona pamegeuka kuwa na shimo na nywele za mahali hapo zimegeuka kuwa nyeupe, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; huo ni ugonjwa wa ukoma ambao umetokana na jipu. 21Lakini kama kuhani atamwangalia huyo mtu na kuona kuwa nywele za mahali hapo si nyeupe na wala hakuna shimo, ila pamefifia, basi, atamtenga huyo mtu kwa muda wa siku saba. 22Kama ugonjwa huo utaenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; sehemu hiyo ina ugonjwa. 23Lakini, kama ile sehemu haijaenea, basi, lile ni kovu la jipu tu. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi.
24“Au, Iwapo kuna mahali palipoungua na ile nyama mbichi imegeuka kuwa nyekundu-nyeupe au ni nyeupe, 25kuhani atapaangalia. Kama akiona kuwa nywele zimegeuka kuwa nyeupe na pana shimo, basi, huo ni ukoma. Ukoma huo umejitokeza kwa njia ya mahali hapo palipoungua. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; kwani anao ugonjwa wa ukoma. 26Lakini kama kuhani akiona kuwa nywele za mahali hapo si nyeupe na hakuna shimo ila pamefifia, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda wa siku saba. 27Siku ya saba kuhani atamwangalia. Kama umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; kwani anao ugonjwa wa ukoma. 28Lakini, kama ile alama haijaenea, ila imefifia, huo ni uvimbe uliotokana na kuungua; basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi; kwani hilo ni kovu la kuungua.
29“Kama mtu yeyote mwanamume au mwanamke, ana kidonda kichwani au kidevuni, 30kuhani atauangalia ugonjwa huo. Iwapo kuhani ataona kuwa kuna shimo na nywele ni manjano na nyembamba, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; kwani huo ni upele na ni ukoma wa kichwa au wa kidevu. 31Kama kuhani ataona kuwa hakuna shimo na nywele si nyeusi, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda wa siku saba. 32Siku ya saba kuhani atakiangalia kile kidonda. Kama kidonda hicho hakijaenea na hakuna nywele zenye rangi ya manjano wala hakuna vipele vyovyote mahali hapo, basi, 33mtu huyo atanyoa nywele au ndevu zake. Lakini mahali pale penye vipele hatapanyoa. Kisha kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda mwingine wa siku saba. 34Siku ya saba, kuhani ataviangalia vile vipele. Iwapo kuhani ataona kuwa vipele hivyo havikuenea kwenye ngozi na wala havikwenda ndani ya ngozi, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa safi. Mtu huyo atafua mavazi yake, naye atakuwa safi. 35Lakini iwapo vipele hivyo vimeenea baada ya kutakaswa, 36mtu huyo ataangaliwa na kuhani na ikiwa vimeenea kwenye ngozi, kuhani hatahitaji kutafuta nywele zenye rangi manjano; mtu huyo atakuwa najisi. 37Lakini iwapo kuhani ataona kuwa vile vipele vimepona na nywele nyeusi zimeota mahali hapo, basi, vidonda hivyo vimepona, basi, mtu huyo ni safi. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi.
38“Kama mtu yeyote, awe mwanamume au mwanamke, ana alama nyeupe mwilini mwake, 39kuhani atamwangalia mtu huyo. Iwapo kuhani ataona kuwa alama hizo ni nyeupe kiasi, huo ni upele wa kawaida; mtu huyo ni safi.
40“Kama mwanamume amepata upara, yeye ni safi kwani ana upara tu. 41Iwapo upara huo umetanda tangu nyuma mpaka mbele mtu huyo ana upara tu na yu safi. 42Lakini kama kwenye kichwa penye upara au kwenye paji la uso penye upara kuna alama nyekundu-nyeupe, huo ni ukoma unaotokea kwenye upara wake kichwani au kwenye paji lake. 43Kuhani atamwangalia. Iwapo kuhani ataona kuwa huo uvimbe ni mwekundu-mweupe kwenye upara au kwenye paji lake na unaonekana kama ukoma kwenye ngozi yake, 44basi, mtu huyo ana ukoma; yeye ni najisi. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ugonjwa wake upo kwenye kichwa chake.
45“Mwenye ukoma yeyote atavaa nguo zilizochanika, nywele zake hatazichana, na mdomo wake wa juu ataufunika na atapaza sauti akisema, ‘Mimi ni najisi, mimi ni najisi.’ 46Ataendelea kuwa najisi kwa muda wote alio na ugonjwa huo. Yeye ni najisi; naye atakaa peke yake nje ya kambi.”

Sheria kuhusu upele katika nguo

47“Kama kuna namna ya upele wa ukoma kwenye vazi, liwe la sufu au kitani, 48vazi hilo liwe limefumwa au limesokotwa kwa kitani au sufu au ni vazi la ngozi ya aina yoyote ile, 49iwapo upele huo una rangi ya kijani au nyekundu katika vazi hilo, basi, vazi hilo lina upele. Kwa hiyo ni lazima kumwonesha kuhani. 50Kuhani atauangalia upele huo na kuliweka vazi hilo kando kwa muda wa siku saba. 51Siku ya saba atauangalia upele huo. Ikiwa upele huo umeenea katika vazi hilo, liwe ni la kufuma au kusokotwa au la ngozi au la ngozi ya aina yoyote ile, vazi hilo lina upele. Hivyo vazi hilo ni najisi. 52Kuhani atalichoma moto vazi hilo kwani lina namna ya upele wa ukoma.
53“Kama kuhani ataona kuwa upele haukuenea katika vazi, basi, 54ataamuru vazi hilo lifuliwe na kuwekwa kando kwa muda mwingine wa siku saba. 55Kuhani ataliangalia hilo vazi baada ya kuoshwa. Ikiwa ile alama haijabadilika rangi yake hata ingawa upele haukuenea, basi, vazi hilo ni najisi. Vazi hilo utalichoma moto, iwe alama ya upele ipo nyuma au mbele ya vazi hilo.
56“Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kufuliwa, basi atararua ile sehemu iliyo na namna ya upele wa ukoma. 57Kisha, ikiwa hiyo alama inaonekana tena baadaye katika vazi lililofumwa au lililosokotwa au katika kitu chochote cha ngozi, basi upele umeenea. Hapo vazi hilo utalichoma moto. 58Lakini vazi ambalo upele umetokea baada ya kulifua itabidi lifuliwe mara ya pili na hivyo lipate kuwa safi.” 59Hiyo ni sheria kuhusu namna ya upele wa ukoma unaotokea katika vazi la sufu au kitani au lililofumwa au lililosokotwa au la ngozi. Kwa njia hiyo mtaweza kupambanua kati ya vazi lisilo najisi na lile lililo najisi.

Mambo Ya Walawi 13;1-59

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 12 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..12...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Asante Mungu wetu Baba yetu,Asante kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako usiku na siku zote umekuwa nasi Jehovah..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala nguvu zetu ni kwa Neema/Rehema yako tuu Mungu wetu sisi kuwepo leo hii na kuweza kufanya yote haya tufanyayo..

Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Yahweh..

Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Utuepushe na majaribu ya yule mwovu na kazi zake..Utuokoe na kutufunika na Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase  Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Tukaanze nawe Bwana wetu katika wiki hii..yote tunayoenda kufanya/kutenda yakaendane na matakwa yako Jehovah..

ukaonekane kwenye maisha yetu Yahweh..!ukatupe hekima,Busara katika kuamua na kutenda,tukapate kutambua/kujitambua..
Tukaelewe na kulijua Neno lako,Tukafuate na  tukatii sheria zako na Amri zako

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Kila kuhani mkuu ambaye huchaguliwa miongoni mwa watu hupewa jukumu la kushughulikia mambo ya Mungu kwa niaba ya watu, kutolea zawadi na tambiko kwa ajili ya dhambi. Maadamu yeye mwenyewe ni dhaifu, anaweza kuwatendea kwa huruma wale wasiojua kitu na wanaofanya makosa. Kwa sababu hiyo anapaswa kutoa tambiko si tu kwa ajili ya watu, bali pia kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe. Hakuna mtu awezaye kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Kila mmoja huteuliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kama alivyokuwa Aroni. Hali kadhalika naye Kristo; yeye hakujitwalia mwenyewe heshima ya kuwa kuhani mkuu, bali Mungu alimteua na kumwambia: “Wewe ni Mwanangu; mimi leo nimekuwa baba yako.” Alisema pia mahali pengine: “Wewe ni kuhani milele, kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” Yesu alipokuwa anaishi hapa duniani, kwa kilio kikuu na machozi, alisali na kumwomba Mungu ambaye alikuwa na uwezo wa kumwokoa kifoni; naye alisikilizwa kwa sababu ya kumcha Mungu. Lakini, ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso. Na alipofanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii, naye Mungu akamteua kuwa kuhani mkuu kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.
Ukatuongoze ee Mungu wetu na ukatubariki na kubariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi utupe neema ya kuwabariki wenyekuhitaji..

 Neno lako likawe Mwanga kwenye maisha yetu likawe faida na likatufae sisi na wengine pia..
Wale walio asi wakapate kurudi kundini na kuwa pamoja katika kuamini na kujifunza zaidi..



Tunayo mengi ya kusema juu ya jambo hili, lakini ni vigumu kuwaelezeni, kwa sababu nyinyi si wepesi wa kuelewa. Kwa wakati huu nyinyi mngalipaswa kuwa waalimu tayari, lakini mnahitaji bado mtu wa kuwafundisheni mafundisho ya mwanzo juu ya neno la Mungu. Mnahitaji maziwa badala ya chakula kigumu. Kila anayepaswa kunywa maziwa ni mtoto bado, hajui uadilifu ni nini. Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu waliokomaa, waliofunzwa kwa vitendo kubainisha mema na mabaya.

.Baba wa Mbinguni ukaonekane kwenye Maisha yetu na tusipungukiwe na mahitaji yetu..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako,Tukiamini wewe ni Mungu wetu hatuna Mungu mwingine..
Yote tuliyoyanena na kutonena Baba unayajua na unatujua kuliko tunavyojijua..
Mungu wetu ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Sifa na Utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..

Amina..!
Mungu aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake..
Niwashukuru sana kwakunisoma/kupita hapa..
Nawapenda.

Kuwatakasa wanawake baada ya kujifungua

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Waambie watu wa Israeli hivi: Mwanamke akipata mimba, akajifungua mtoto wa kiume, atakuwa najisi kwa muda wa siku saba kulingana na siku zake zihusikanazo na hali ya wanawake. 3#Taz Mwa 17:12; Luka 2:21 Mtoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane. 4Kisha mama mtoto ataendelea kuwa najisi kwa muda wa siku thelathini na tatu. Wakati huo, kamwe asiguse chochote kilichowekwa wakfu wala kuingia mahali patakatifu mpaka siku za kutakasika kwake zitakapotimia. 5Lakini, kama amejifungua mtoto wa kike, basi, atakuwa najisi kwa muda wa majuma mawili kama ilivyo anapokuwa katika siku zake. Ataendelea katika kutakasika kwake kwa muda wa siku sitini na sita.
6“Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, iwe amepata mtoto wa kiume au wa kike, atamletea kuhani mlangoni mwa hema la mkutano mwanakondoo wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kinda la njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi. 7Kuhani atamtolea mbele ya Mwenyezi-Mungu na kumfanyia huyo mama ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu. Hivyo huyo mwanamke atakuwa safi kutokana na damu yake. Huo ni mwongozo kuhusu mwanamke yeyote anayejifungua mtoto wa kiume au wa kike.
8 # Taz Luka 2:24 “Kama hawezi kutoa mwanakondoo, basi, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa; mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuondolea dhambi. Kuhani atamfanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.”

Mambo Ya Walawi12;1-8


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 9 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..11...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Ni siku nyingine tena Mungu ametuchagua na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala si kwa nguvu zetu,si kwamba sisi ni wema sana au wazuri mno kuliko wengine ambao leo hii wapo vitandani,wapo waliotangulia/kufa,wengine wapo hoi hata kuita Mungu au kutubu wameshindwa,wapo wanaotamani kuandika/kusoma kama si kuongea au kuacha wosia/usia kwa wapendwa wao..
Sisi tumempa nini Mungu wetu? ni kwa Neema/Rehema zake Mungu sisi kuwepo na kuwa hivi tulivyo..
Tumshukuru Mungu kwa wema na Fadhili zake na tukatumie nafasi hii aliyotupa vizuri  kwa kutenda yaliyo mema na tuzidi kumtafuta kwa maana anapatikana..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yake..
Asante Mungu wetu na Baba yetu uliye Mbinguni..
Asante kwa kulinzi wako wakati wote na kutuamsha salama..
Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mungu wetu, kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakuju/kutojua..Mfalme wa Amani..
Tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe nasi waliotukosea..
utuepushe na Majaribu Mungu wetu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake..ututakase na kutufunika kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu pia tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi.
Tunaomba utubariki na kubariki vyote tunavyoenda kufanya/kutenda,na ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..
Maisha yetu yapo mikononi mwako Mungu wetu..
yote tuliyoyanena na tusiyo yanena Mungu wetu unayajua na kutujua kuliko tunavyojijua sisi..
Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi utupe neema ya kuwabariki wanaohitaji..
Baba wa Mbinguni  tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako..



Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo na ndugu yake Yakobo, nawaandikia nyinyi mlioitwa na Mungu na ambao mnapendwa naye Mungu Baba, na kuwekwa salama kwa ajili ya Yesu Kristo. Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.

Tunarudisha Sifa na utkufu ni wako,Tunakushukuru na kukusifu Daima..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu  hata Milele...
Amina..!!



Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta nyinyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake, kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina.


Asanteni sana wapendwa/waungwana kwa kutembelea hapa..
Mungu akawaongoze katika maisha yenu na msipungukiwe katika mahitaji yenu na akawape sawasawa na mapenzi yake..
Sina neno zuri kwenu zaidi ya kuwaombea na kuwaambia..
Nawapenda.

Wanyama najisi na wasio najisi
(Kumb 14:3-21)

1Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, 2“Wawaambie Waisraeli hivi: 3Kati ya wanyama wote duniani, mmeruhusiwa kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua. 4Lakini msile mnyama yeyote ambaye hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika sehemu mbili, au ambaye kwato zake zimegawanyika lakini hacheui. Msile ngamia, kwani hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika sehemu mbili. Kwenu huyo ni najisi. 5Pelele msimle; yeye hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika; kwenu huyo ni najisi. 6Sungura msimle; yeye hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika; kwenu huyo ni najisi. 7Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi. 8Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao wala msiguse mizoga yao.
9“Samaki yeyote wa baharini au mtoni mwenye mapezi na magamba, mnaweza kumla. 10Lakini chochote kinachoishi baharini au mitoni, ambacho hakina mapezi wala magamba, yaani viumbe vyote viendavyo majini na viumbe vingine vyote viishivyo majini ni najisi kwenu. 11Viumbe hivyo vitakuwa daima najisi kwenu. Msile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao kwani ni najisi. 12Chochote kinachoishi majini ambacho hakina mapezi na magamba ni najisi kwenu.
13“Ndege wote wafuatao ni najisi kwenu; hivyo msile: Tai, furukombe, kipungu, 14mwewe, aina zote za kozi, 15aina zote za kunguru, 16mbuni, kirukanjia, dudumizi, aina zote za kipanga, 17bundi, mnandi, bundi kubwa, 18mumbi, mwari, mderi, 19korongo, aina zote za koikoi, hudihudi na popo.
20“Wadudu wote wenye mabawa na waendao kwa miguu minne, hao ni najisi kwenu. 21Lakini, baadhi ya wadudu wenye mabawa na wanakwenda kwa miguu minne ya kurukia ardhini mnaweza kula. 22Hao ni: Kila aina ya nzige, kila aina ya senene, kila aina ya panzi na kila aina ya parare. 23Lakini wadudu wengine wote wenye mabawa na miguu minne ni najisi kwenu.
24“Kugusa wanyama fulanifulani humfanya mtu kuwa najisi; yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni. 25Mtu akichukua sehemu ya mizoga yake atakuwa najisi mpaka jioni, na mavazi yake ni lazima yafuliwe. 26Mtu yeyote akigusa mnyama mwenye kwato zilizogawanyika lakini hacheui, mtu huyo atakuwa najisi. 27Wanyama wote waendao kwa vitanga vyao ingawa wana miguu minne, ni najisi kwenu; na yeyote atakayegusa mzoga wa mnyama kama huyo atakuwa najisi mpaka jioni. 28Mtu yeyote anayebeba mzoga atakuwa najisi, naye atasafisha mavazi yake. Hao ni najisi kwenu.
29“Viumbe vifuatavyo ni najisi kwenu: Kicheche, panya, kila aina ya mjombakaka, 30guruguru, kenge, mijusi, goromwe, na kinyonga. 31Hao wote ni najisi kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa najisi mpaka jioni. 32Ikiwa mzoga wa viumbe hao unakiangukia kitu chochote, kiwe ni kifaa cha mbao au vazi au ngozi au gunia au chombo chochote kitumiwacho kwa kusudi lolote lile, chombo hicho kitakuwa najisi mpaka jioni. Ili kukifanya kiwe safi ni lazima kukiosha kwa maji. 33Ikiwa mzoga wake umeangukia chombo cha udongo, basi, chochote kilicho ndani ya chombo hicho ni najisi na lazima chombo hicho kivunjwe. 34Chakula au kinywaji chochote kilichokuwa ndani ya chombo hicho kitakuwa najisi. 35Kila kitu ambacho sehemu ya mzoga imekiangukia, kitakuwa najisi. Ikiwa ni tanuri au jiko, ni lazima kivunjwe. Vitakuwa najisi navyo ni najisi kwenu. 36Hata hivyo, kisima au chemchemi ya maji vitakuwa safi. Lakini chochote kinachogusa mzoga kitakuwa najisi. 37Iwapo sehemu ya mzoga inaziangukia mbegu za kupanda, mbegu hizo hazitakuwa najisi. 38Lakini ikiwa mbegu zimetiwa katika maji ili kuota na sehemu yoyote ya mzoga ikaziangukia, basi, mbegu hizo ni najisi kwenu.
39“Iwapo mnyama yeyote mnayeruhusiwa kula, anakufa mwenyewe, yeyote atakayegusa mzoga wake, atakuwa najisi mpaka jioni. 40Mtu yeyote akila nyama ya mzoga huo atafua mavazi yake na atakuwa najisi mpaka jioni. Na yeyote atakayebeba mzoga huo, atafua mavazi yake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41“Kiumbe chochote kitambaacho duniani ni najisi kwenu, kamwe msikile. 42Chochote kiendacho kwa tumbo lake, chochote kiendacho kwa miguu yote minne au nyayo nyingi, naam, chochote kitambaacho, kamwe msikile kwa maana ni najisi kwenu. 43Hivyo msije mkawa najisi kwa kula viumbe vitambaavyo na hivyo mkawa najisi. 44#Taz Lawi 19:21; 1Pet 1:16 Kwa kuwa mimi Mwenyezi-Mungu ndimi Mungu wenu, jiwekeni wakfu na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mtakatifu. 45Kwa kuwa mimi Mwenyezi-Mungu ndimi niliyewatoa nchini Misri ili niwe Mungu wenu; kwa hiyo muwe watakatifu kwa maana mimi ni mtakatifu.”
46Hiyo basi, ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege na viumbe vyote hai ambavyo huishi majini na nchi kavu, 47ili kupambanua kati ya kisicho najisi na kilicho najisi; kinachoweza kuliwa na kisichoweza kuliwa.

Mambo Ya Walawi11;1-47


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 8 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..10...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote..
Asante Baba wa Mbinguni,Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo,Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Yahweh..!Jehovah..!Jehovah nissi..!Jehovah Shammah..!Jehovah Jireh..!Jehovah Rapha..! Jehovah Roi..!Jehovah Shalom..!!
Hakuna kama wewe Baba wa Mbinguni wewe ni Alfa na Omega,Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Unatosha Mungu wetu...!!

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako,
Asante kwa kutulinda usiku na wakati wote na umetuamsha salama..
Asante kwakutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..

Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachili mikononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwa kuwaza,kunena,kutenda,kujua/kutojua..Baba wa Mbinguni Tunaomba nasi utupe Neema ya kuiweza kuwasamehe waliotukosea..

Utuepushe na majaribu, utuokoe na yule mwovu na kazi zake..Mungu wetu ututakase na utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..

Mungu wetu tunaomba uwabariki na kuwatendea,Ukawaguse na mkono wako wenye nguvu Yatima na Wajane na ukawaponye kimwili na kiroho wote wanaotaabika kwa Shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokwenye vifungo mbalimbali Baba ukawafungue na wote waliokata tamaa,wenye hofu/mashaka wakapate tumaini na wakawe na Amani ya moyo na ukawatendee sawa sawa na mapenzi yako.


Wapendwa tumrudishie Sifa na Utukufu Mungu wetu,Tuwe na wakati wa kukumbuka na Kumshukuru Mungu kwa Mema meengi aliyotutendea/anayotutendea..Tusiwe watu wa kulalamika tuu kila siku na kusahau wema wa Mungu..Tunasahau mangapi ametenda kwenye maisha yetu,Tusiwe wepesi wa kukumbuka mapito/majaribu tuu na kumuasi Mungu wetu kwamba ametuacha..Tukumbuke wapi tulipotoka na wapi tunaenda,tukumbuke wema na fadhili zake,tukumbuke si kwamba mimi/wewe ni wema sana na tunaweza yote hayo kwa uwezo wetu..
Tukumbuke kwa Neema/Rehema zake ndiyo tunaishi,Tunapata mahitaji yetu wala si kwamba tuna nguvu ya kufanya kazi/biashara au kwa akili zetu wenyewe pasipo maarifa aliyotupa Mungu ndiyo tunafanikiwa..


Ee Mungu wetu Tunakushukuru katika yote,Tunakushukuru kwa uweza wako na kutupa sisi nafasi ya kufanya/kutenda yote haya..

Tusipo weza kumshukuru Mungu wetu kwa kidogo tulichonacho jee tutakumbuka kwa kikubwa..?Tusijilinganishe na maisha ya wengine na kulalamika Mungu mbona mimi hivi na huyu vile,Tumshukuru kwa hili kwanza na tumuombe na atupe maarifa,ubunifu na tukatumie vyema karama alizotupa...
Tumkabidhi maisha yetu na kuomba muongozo huku nasi tukijibidisha..


Ee Mwenyezi-Mungu, unifundishe kutii masharti yako; nami nitayashika mpaka mwisho. Unieleweshe nipate kuishika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote. Uniongoze katika njia ya amri zako, maana humo napata furaha yangu. Unipe ari ya kuzingatia maamuzi yako, na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa. Uniepushe, nisifuate mambo ya upuuzi; unioneshe njia yako, unipe uhai. Unitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako; ahadi unayowapa wale wanaokuheshimu. Uniokoe na lawama ninazoogopa; maana maagizo yako ni mema. Natamani sana kuzitii kanuni zako; unijalie uhai maana wewe ni mwadilifu.
Mungu wetu yu Mwema sana...!
Ee Mungu wetu ukatuongoze na kutuepusha na mambo yote yasiyokupendeza..
Ee Mungu wetu ukatupe kujua na kulielewa vyema Neno lako..

Ee Mwenyezi-Mungu, upokee sala yangu ya shukrani; na kunifundisha maagizo yako.
Asante Mungu wetu Tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Tukiamini na kukusifu daima..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukukufu hata Milele..
Amina..!
Mungu aendelee kuwabariki..
Asanteni sana kwakunitembea/kunisoma..
Nawapenda sana.





Dhambi ya Nadabu na Abihu

1Nao Nadabu na Abihu, wanawe Aroni, walichukua kila mmoja chetezo chake, wakaweka moto na ubani, wakamtolea Mwenyezi-Mungu moto najisi, ambao haukulingana na agizo lake Mwenyezi-Mungu. 2Basi, moto ukatokea mbele ya Mwenyezi-Mungu, ukawateketeza hao vijana, wakafa mbele yake. 3Hapo, Mose akamwambia Aroni, “Kwa tukio hili Mwenyezi-Mungu amekuonesha maana ya kile alichosema: ‘Nitajionesha kuwa mtakatifu miongoni mwa wale walio karibu nami; nitatukuzwa mbele ya watu wote!’” Aroni akanyamaza kimya.
4Basi, Mose akawaita Mishaeli na Elsafani, wanawe Uzieli, baba mdogo wa Aroni, akawaambia waje kuondoa maiti za ndugu zao maskani na kuzipeleka nje ya kambi. 5Wakachukua maiti za ndugu zao na kuzipeleka nje ya kambi wakiwa wamevaa mavazi yao, kama Mose alivyoamuru. 6Kisha Mose akamwambia Aroni na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msivuruge nywele zenu na wala msirarue mavazi yenu kuomboleza, la sivyo mtakufa na kuiletea jumuiya yote ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu. Lakini ndugu zenu yaani jumuiya yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo aliouleta Mwenyezi-Mungu. 7Msitoke nje ya mlango wa hema la mkutano, la sivyo mtakufa; kwani mafuta ya kupaka ya Mwenyezi-Mungu yangali juu yenu.” Aroni na wanawe wakafanya kama Mose alivyosema.
8Mwenyezi-Mungu aliongea na Aroni, akasema, 9“Mnapoingia ndani ya hema la mkutano, wewe na wanao msinywe divai wala kileo chochote, la sivyo mtakufa. Hii itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote. 10Ni lazima mtofautishe kati ya mambo matakatifu na mambo yasiyo matakatifu, kati ya mambo najisi na yasiyo najisi. 11Mtawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Mose.”
12 # Taz Lawi 6:14-18 Mose akamwambia Aroni na wanawe waliosalia: Eleazari na Ithamari, “Chukueni ile sehemu ya sadaka ya nafaka iliyosalia kutoka sadaka anazotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto; muile karibu na madhabahu bila kutiwa chachu kwa sababu ni takatifu kabisa. 13Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazawa wako kutoka katika sadaka anazotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. Hivyo ndivyo nilivyoamriwa. 14#Taz Lawi 7:30-34 Lakini kidari ambacho hufanywa nacho ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu na mguu unaotolewa sadaka kama ishara, mnaweza kula mahali popote pasipo najisi. Utakula wewe, na watoto wako wa kiume na wa kike. Vitu hivyo umepewa kama haki yako na ya wazawa wako kutoka sadaka za amani za watu wa Israeli. 15Ule mguu uliotolewa na kidari cha sadaka ya kufanyia ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu watavileta pamoja na sadaka za mafuta zitolewazo kwa moto, ili kufanya ishara ya kuvitolea mbele ya Mwenyezi-Mungu, viwe sadaka ya kutolewa kwa ishara. Hivyo vitakuwa vyako pamoja na wanao; ni haki yenu milele kama Mwenyezi-Mungu alivyoamuru.”
16Basi, Mose alichunguza kwa makini kuhusu mbuzi mmoja aliyetolewa sadaka ya kuondoa dhambi, kumbe akagundua kuwa alikwisha teketezwa. Hivyo akawakasirikia sana Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia, akawauliza, 17#Taz Lawi 6:24-26 “Kwa nini hamkumla katika mahali patakatifu kwa vile huyo ni kitu kitakatifu kabisa na mlikuwa mmepewa huyo ili kuondoa hatia ya jumuiya na kuwafanyia ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu? 18Tena, kwa vile damu yake haikuletwa ndani ya mahali patakatifu, ni dhahiri iliwapasa kumla ndani ya mahali patakatifu kama nilivyoamuru.” 19Aroni akamwambia Mose, “Tazama, leo wametolea sadaka yao ya kuondoa dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele ya Mwenyezi-Mungu; hata hivyo mambo haya yamenipata! Tena kama ningekula ile sadaka ya kuondoa dhambi hivi leo, je, ingekubalika mbele ya Mwenyezi-Mungu?” 20Mose aliposikia hayo, akaridhika.

Mambo Ya Walawi10;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.