Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 7 October 2016

Mahojiano na Rahima Shaaban. Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Ubunifu wa Beautiful Jamila




Kwanza Production

 Beautiful Jamila ilianzishwa mwaka 2013 na Rahima Shabani na makao makuu ni Atlanta Georgia.

Inajihusisha na harakati za kutangaza tamaduni za kiSwahili na kiAfrika.

Mwanzilishi wake aliungana nasi studio kuzungumza mengi kuhusu yeye, kampuni yake na tamasha lijalo




Wednesday 21 September 2016

Kipindi cha Reggae Time Pride Fm Sept 17 2016.....Mahojiano na Innocent Galinoma


Karibu katika kipindi cha REGGAE TIME ya Pride Fm Mtwara Tanzania.

Na leo, ni mazungumzo yangu na Innocent Galinoma ambaye alikuwa mkarimu sana kufika Kilimanjaro Studios kwa mahojiano.



Ni kuanzia saa tisa kamili alasiri kwa saa za Afrika Mashariki, mbili kamili kwa Marekani Mashariki

Jiunge nasi kupitia 87.8 Fm kwa mikoa ya kusini, ama www.878pridefm.com ama kupitia TuneIn, bofya tun.in/seTTx.

Tuesday 13 September 2016

Kipindi Cha Jukwaa Langu Sep 12 2016....Tetemeko Bukoba


Katika kipindi cha JUKWAA LANGU hii leo, tulizungumzia janga kuu la Tetemeko la ardhi nchini Tanzania
Wadau
Baraka Galiatano wa BukobaWadau Blog na Erick Kimasha walijiunga nasi
kwa njia ya Skype kutoka Tanzania kutupa taswira ya nini kilitokea, vipi
kilipokelewa na maendeleo tangu Sept 10 na hali ilivyo hivi sasa mjini
humo.
Pia tuliungana na mmoja wa wanaharakati ambao wameanzisha mfuko maalum kuchangia wahanga wa tetemeko hilo Agnetta .



Ungana nasi kuanzia saa 11 kamili jioni majira ya Marekani Mashariki (5:00pm ET) kupitia www.kwanzaproduction.com ama kupitia TuneIn tun.in/sfeLX
Kwa walio Marekani na Canada piga 240 454 0093

Karibuni

Tuesday 30 August 2016

Kipindi cha JUKWAA LANGU Aug 29 2016 (Pt 1)...Demokrasia Tanzania


Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu TANZANIA ya sasa na ile tuitakayo.

Katika kipindi cha wiki hii, mbali na habari mbalimbali zilizotawala vyombo vya habari, pia wasikilizaji walipata nafasi ya kutoa maoni kulingana na mambo mbalimbali yanayoendelea nchini Tanzania na ukuaji wa Demokrasia ya nchi yetu.

KARIBU

Mahojiano na Prof Julius Nyang'oro katika kipindi cha JUKWAA LANGU


Profesa Julius Nyang'oro ni Mwalimu, mtaalam wa sayansi ya siasa na mwanasheria.

Amekuwa mwalimu tangu mwaka 1977 nchini Tanzania na hapa nchini Marekani.

Ni mwandishi wa vitabu zaidi ya 14, vingi vikiigusia Tanzania kwa namna moja ama nyingine. Moja ya vitabu alivyoandika, na ambavyo vilimtambulisha zaidi kwa jamii ya waTanznia, ni kumhusu Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete. Ambapo ameandika vitabu viwili kumhusu.

Prof Nyang'oro alikuwa mkarimu sana kuungana nasi kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU Jumatatu ya Agosti 29, 2016 kuzungumzia mambo mbalimbali kuihusu Tanzania akiwa mwandishi, mwalimu, mtaalamu wa mausala ya siasa na
mwanasheria

KARIBU




Thursday 4 August 2016

Wawakilishi wa Tanzania katika YALI 2016 wazungumza kuhusu kongamano lao Washington DC

Stanley Magesa (mjasiriamali) akifafanua jambo ndani ya studio kuhusu YALI 2016


Aug 3, 2016 tulipata fursa ya kutembelewa na kuhojiana na baadhi ya
Watanzania wanaowakilisha kwenye mkutano wa Mandela Washington
Fellowship - Young African Leaders Initiative (YALI) 2016 waliomaliza
mkutano wao hapa Washington DC

Walikuwa wakarimu sana kujiunga nasi Studio na kuzungumza nasi kuhusu mambo mbalimbali

Karibu uwasikilize



Heri Emmanuel (kati kutoka Mwanza) akieleza jambo huku Tusekile Mwakalundwa ( Mhadhiri na Mwanasheria kutoka Arusha) akisikiliza kwa makini. Kulia ni Mubelwa Bandio wa Kwanza Production na Vijimambo Radio
Baadhi ya wawakilishi wa YALI 2016 kutoka Tanzania, wajasiriamali Stanyey Magesa (Mwanza), Simon Malugu (Morogoro) na Lusajo Mwaisaka (Dar) wakiwa kwenye mahojiano Kilimanjaro Studio
Mshiriki wa YALI 2016 Heri Emmanuel (Mwanza) kulia akaifafanua jambo huku akisikilizwa na mshiriki mwenzake ambaye pia ni Mhadhiri na Mwanasheria Tusekile Mwakalundwa (Arusha) na mjasiriamali na Lusajo Mwaisaka (kutoka Dar)



Sunday 24 July 2016

Muendelee na Jumapili nyema;Burudani-Bado Sijafika,Kina Cha Upendo Wako,Twaokolewa kwa Neema - Kijitonyama choir



Wapendwa/Waungwa natumaini Jumapili inaendelea vyema..
Basi muendelee kuwa na Amani,Furaha,Baraka na msipungukiwe na
kila lililojema Mungu awe nanyi daima.






Kuumbwa ulimwengu
1Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia. 2Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji.
3Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa. 4Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza,5mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza.
   



    Neno La Leo;Mwanzo 1:1-31



6Mungu akasema, “Anga liwe katikati ya maji, liyatenge maji sehemu mbili.” 7Mungu akalifanya anga, akayatenga maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo. 8Mungu akaliita anga “Mbingu.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili.





9Mungu akasema, “Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, nchi kavu itokee.” Ikawa hivyo. 10Mungu akapaita mahali pakavu “Nchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.







11Kisha Mungu akasema, “Nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu.” Ikawa hivyo. 12Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. 13Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tatu.
14Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka, 15na ingae angani na kuiangazia dunia.” Ikawa hivyo. 16Basi, Mungu akafanya mianga miwili mikubwa; ule mkubwa utawale mchana na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. 17Mungu akaiweka mianga hiyo angani iiangazie dunia, 18ipate kutawala mchana na usiku, na kuutenga mwanga na giza. Mungu akaona kuwa ni vyema. 19Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne.


20Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.” 21Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema.22Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni, muongezeke, muyajaze maji ya bahari; nao ndege waongezeke katika nchi.” 23Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tano.



24Mungu akasema, “Nchi na itoe aina zote za viumbe hai, wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo na wanyama wa porini wa kila aina.” Ikawa hivyo. 25Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema.
26Kisha Mungu akasema, “Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; atawale samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vitambaavyo.” 27 Basi, Mungu akaumba mtu kwa mfano wake; naam, kwa mfano wake Mungu alimuumba. Aliwaumba mwanamume na mwanamke. 28Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.”


29Kisha Mungu akasema, “Tazama, nawapeni kila mmea duniani uzaao mbegu, na kila mti uzaao matunda yenye mbegu; mbegu zao au matunda yao yatakuwa chakula chenu. 30Nao wanyama wote duniani, ndege wote wa angani, viumbe vyote vitambaavyo, naam, kila kiumbe chenye uhai, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikawa hivyo. 31Mungu akaona kila kitu alichokifanya kuwa ni chema kabisa. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya sita.


Biblia Habari Njema


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.