Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 20 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..18...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu katika yote..
Mungu wetu,Baba yetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo ni mali yako,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako Baba..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote..
Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendele kuiona leo hii..
Mfalme wa Amani tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako..

Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
utuepushe katika majaribu na utuokoe na  yule mwovu na kazi zake zote..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu na utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..


Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga. Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa nyinyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni. Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu. Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake. Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao. Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena. Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika. Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, na kutupa jukumu la kuwapatanisha watu naye. Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye. Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi nyinyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu. Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukapate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..

Ee Mungu wetu Tunakutukuza na kutukuza Jina lako..
Ee Mungu wetu tunakusifu na kusifu Jina lako..
Ee Mungu wetu asante kwakutupenda kwanza..
Ee Mungu wetu utupe neema ya kupendana nasi,Utupe neema ya kushinda majaribu,Utupe neema ya kufuata Neno lako,Sheria na Amri zako..
Ee Mungu wetu utuepushe na Kiburi,choyo,chuki,majivuno,kujisifu,kujitukuza,dharau,masimango,wivu na kuneneana mabaya..
Ukatupe macho ya Rohoni na masikio ya kusikia..Mdomo wa kukusifu na kutangaza Neno lako,Hekima,Busara,Utuwema,Upendo,Maarifa,Ubunifu na tukatambue nini chakufanya/tunatakiwa kufanya..ukatuonyeshe njia iliyo yako na kila mmmoja akajue jukumu lake na kazi zake ulizomtuma hapa Duniani..

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Ukaibariki  siku hii na ukatubariki katika yote ..
Vyote tunavyoenda kutenda/kugusa na ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Asante Mungu wetu wewe watosha..

Hakuna na  hatokuwepo kama wewe..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako Mungu wetu..
tuliyoyanena na tusiyoyanena Mungu wetu unayajua na kutujua sisi zaidi ya tunavyojijua wenyewe..
Sifa na Utukufu ni wako..Tunakushukuru Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..

 Amina...!

Asanteni sana sana Wapendwa kwa kuwa nami/kunisoma..

Mungu akawaongoze kwa kila jambo..
Nawapenda.

Matendo maovu ya ndoa

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Waambie watu wa Israeli hivi: Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu. 3Kamwe msifanye kama wafanyavyo watu wa nchi ya Misri ambako mlikaa; wala msifanye kama wafanyavyo watu wa nchi ya Kanaani ambako nawapeleka. Kamwe msifuate mitindo yao. 4Nyinyi mtafuata maagizo yangu na kuyashika masharti yangu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu. 5#Taz Neh 9:29; Eze 18:9; 20:11-13; Luka 10:28; Roma 10:5; Gal 3:12 Kwa hiyo, ili mtu apate kuyaokoa maisha, mnapaswa kuyashika masharti yangu na maagizo yangu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
6“Mtu yeyote wa Israeli haruhusiwi kumkaribia mtu wa jamaa yake wa karibu ili kulala naye. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu. 7Kamwe usimvunjie heshima baba yako kwa kulala na mama yako aliyekuzaa. Usimwaibishe; yeye ni mama yako. 8Kamwe usimvunjie heshima baba yako kwa kulala na mmoja wa wake zake. Hao ni mama zako. 9Kamwe usilale na dada yako, awe ni dada yako halisi au dada yako wa kambo. 10Kamwe usilale na mjukuu wako, mtoto wa mwanao au binti yako; maana sehemu zao za siri ni kama zako mwenyewe. 11Kamwe usilale na msichana aliyezaliwa na mama yako wa kambo aliyeolewa na baba yako; msichana huyo ni dada yako. 12Kamwe usilale na shangazi yako; kwani huyo ni dada wa baba yako. 13Kamwe usilale na dada wa mama yako; kwani huyo ni mama yako mkubwa au mdogo. 14Kamwe usilale na mke wa baba yako mkubwa au mdogo; huyo ni mama yako. 15Kamwe usilale na mke wa mwanao; huyo ni mkewe mwanao. Kamwe usilale naye. 16Kamwe usilale na mke wa ndugu yako; huyo ni shemeji yako. 17Ukilala na mwanamke, basi, kamwe usilale naye na binti yake, wala wajukuu zake. Hao ni ndugu. Kuwachanganya ni kufanya uovu. 18Kamwe usimwoe dada wa mkeo wakati mke wako yungali hai; hiyo itasababisha ushindani.
19 # Taz Neh 9:29; Eze 18:9; 20:11-13; Luka 10:28; Roma 10:5; Gal 3:12 “Kamwe usilale na mwanamke awapo mwezini. 20#Taz Lawi 20:10 Kamwe usilale na mke wa jirani yako na hivyo kujitia mwenyewe najisi naye.
21 # Taz Lawi 20:1-5 “Kamwe usimtoe mtoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utalikufuru jina langu mimi Mungu wako. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
22 # Taz Lawi 20:13 “Kamwe usilale na mwanamume mwenzio kana kwamba ni mwanamke. Hilo ni chukizo. 23#Taz Kut 22:19; Lawi 15-16; Kumb 27:21 Kamwe usilale na mnyama ili usijitie najisi; mwanamume au mwanamke yeyote kamwe asifanye hivyo; kufanya hivyo ni upotovu.
24“Msijitie najisi kwa kufanya mambo hayo kwani kwa sababu ya mambo hayo nayafukuza mataifa yaliyo mbele yenu kwa vile wao hufanya hayo na kujitia najisi. 25Nchi yao ilitiwa unajisi nami nikaiadhibu, nayo ikawakataa wakazi wake. 26Lakini nyinyi na wageni wanaokaa kati yenu ni lazima kuyashika masharti na maagizo yangu na wala msifanye machukizo hayo. 27Machukizo hayo waliyafanya watu waliokaa katika nchi ya Kanaani kabla yenu, nao wakaitia nchi unajisi. 28Basi, nyinyi msifanye mambo hayo, la sivyo nchi hiyo itawatapika kama ilivyolitapika taifa lililokuwa kabla yenu. 29Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza ni lazima watengwe mbali na watu wao. 30Kwa hiyo shikeni kikamilifu yote ninayowaagiza; msifuate mazoea yoyote ya kuchukiza yaliyofanywa na wale walioishi nchini kabla yenu, msije mkajitia unajisi kwayo. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.”

Mambo Ya Walawi18;1-30


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: