Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 17 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 13...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu ni mwaminifu sana Tumshukuru katika yote..
Yeye aliyetupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..si kwa Uwezo wetu wala nguvu zetu ni kwa Neema/Rehema zake Mungu..
Tuzidi kumsifu na kuamini,Tumaini la kweli,Faraja ipo kwake,Furaha ina yeye,Mwenye mapenzi ya kweli,Asiyeshindwa na Jambo,Mlinzi mkuu,Muumba wetu,Muumba mbingu na Nchi,Mungu wetu,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Yahweh..!!Jehovah..!!Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Alfa na Omega...Hakuna linaloshindikana kwakwe ukiomba na kuamini na kufuata nja zake..
Asante Baba wa Mbinguni kwa  siku hii na kutuamsha salama,Tazama Jana imepita Yahweh..Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine...
Tunakuja mbele zako na tunajinyenyekeza Mfalme wa Amani..Tunaomba ukatubariki na kutulinda,Ukatamalaki na kutuatamia..
Ukabariki tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..Ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka pale msalabani ili sisi tupate kupona..Jehovah..! Ukatakase Akili zetu na Miili yetu tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda na tuwe na kiasi..
Tunakwenda kinyume na Mwovu na kazi zake zote..
Tunajiachilia mikononi mwako Baba..Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe,kwakuwaza/kutenda,kwakujua/kutojua..
Ukatufanye chombo kipya na tukakutumikie sawasawa na mapenzi yako..

Lawi anaitwa kuwa mwanafunzi
(Mat 9:9-13; Marko 2:13-17)

27Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtozaushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, “Nifuate!” 28Naye akaacha yote akamfuata. 29Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake. Na kundi kubwa la watozaushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao. 30Mafarisayo na waalimu wa sheria wakawanungunikia wanafunzi wake wakisema: “Kwa nini mnakula na kunywa pamoja na watozaushuru na wenye dhambi?” 31Yesu akawajibu, “Wenye afya hawamhitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. 32Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, wapate kutubu.[Luka5:27-32]

Baba tunaomba ukawaponye na kuwaokoa wenye Shida/Tabu,Wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao..Tamazama waliovifungoni Baba tunaomba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho ..
Tunashukuru na kukusifu Daima,Tunayaweka haya yote mikononi mwako na kuamini wewe ni Mungu wetu Leo kesho na hata milele.
Amina..!
4Basi, furahini daima katika kuungana na Bwana! Nasema tena: Furahini! 5Upole wenu ujulikane kwa watu wote. Bwana yu karibu. 6Msiwe na wasiwasi juu ya kitu chochote, ila kwa kila hali, mwombeni Mungu katika sala juu ya mahitaji yenu, kwa shukrani. 7Nayo amani ya Mungu ipitayo akili zote za watu italinda salama mioyo na akili zenu katika kuungana na Kristo Yesu.[wafilipi4;4-7]






Kuwaweka wakfu wazaliwa wa kwanza

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Niwekee wakfu wazaliwa wote wa kwanza wa kiume, maana wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa Waisraeli na kila wazaliwa wa kwanza wa wanyama ni wangu.”
Sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu
3Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii mliyotoka nchini Misri ambako mlikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Mwenyezi-Mungu alipowatoa humo kwa mkono wake wenye nguvu. Katika siku hii, kamwe msile mkate uliotiwa chachu. 4Siku hii, mwezi wa kwanza wa Abibu, mtaondoka nchini Misri. 5Na wakati Mwenyezi-Mungu atakapowafikisha katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi ambayo aliwaapia babu zenu kwamba atawapa nyinyi, nchi inayotiririka maziwa na asali, ni lazima muiadhimishe sikukuu hii kila mwaka katika mwezi huu wa kwanza. 6Kwa muda wa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, na mnamo siku ya saba mtafanya sikukuu kwa heshima ya Mwenyezi-Mungu. 7Kwa muda huo wa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Kusiwepo na mikate iliyotiwa chachu, wala chachu yoyote miongoni mwenu na katika nchi yenu yote. 8Siku hiyo mtawaambia watoto wenu kwamba mnafanya hivyo kwa sababu ya jambo alilowafanyia Mwenyezi-Mungu mlipoondoka nchini Misri. 9Adhimisho hilo litakuwa ukumbusho, kama alama katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; ili iwakumbushe daima sheria ya Mwenyezi-Mungu. Maana, Mwenyezi-Mungu amewatoa nchini Misri kwa mkono wenye nguvu. 10Kwa hiyo, mtaadhimisha sikukuu hii kwa wakati uliopangwa, kila mwaka.”

Maelezo kuhusu wazaliwa wa kwanza

11Mose akaendelea kuwaambia watu, “Hali kadhalika, wakati Mwenyezi-Mungu atakapowafikisha katika nchi ya Wakanaani na kuwapeni iwe mali yenu kama alivyowaapia nyinyi na babu zenu, 12Taz Kut 34:19-20; Luka 2:23 lazima kumwekea Mwenyezi-Mungu kila mzaliwa wenu wa kwanza wa kiume. Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mifugo yenu atakuwa wa Mwenyezi-Mungu. 13Lakini mzaliwa wa kwanza wa kiume wa punda utamkomboa kwa kulipa mwanakondoo, la sivyo, utamuua kwa kumvunja shingo. Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa binadamu utamkomboa. 14Kama hapo baadaye mwanao akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia, ‘Kwa nguvu ya mkono wake, Mwenyezi-Mungu alitutoa nchini Misri ambako tulikuwa watumwa. 15Farao kwa ukaidi alikataa kutuachia tuondoke; kwa hiyo Mwenyezi-Mungu alimuua kila mzaliwa wa kwanza nchini Misri, mzaliwa wa kwanza wa binadamu na wa mnyama. Basi, mimi ninamtolea sadaka Mwenyezi-Mungu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mifugo yangu, lakini kila mzaliwa wa kwanza wa wanangu namkomboa.’ 16Jambo hili litakuwa kama alama mkononi mwako au utepe katika paji la uso wako, kwamba Mwenyezi-Mungu alitutoa nchini Misri kwa mkono wenye nguvu.”
Mnara wa wingu na wa moto

17Wakati Farao alipowaachia Waisraeli waende zao, Mungu hakuwapitisha katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa ya karibu. Mungu alisema, “Sipendi watu hawa wabadilishe nia na kurudi Misri wakijua itawabidi kupigana vita.” 18Badala yake, Mungu aliwapitisha Waisraeli katika njia ya mzunguko kupitia jangwani, kuelekea bahari ya Shamu.13:18 bahari ya Shamu: Kiebrania neno kwa neno ni “bahari ya mafunjo”. Waisraeli waliondoka nchini Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
19 Taz Mwa 50:25; Yos 24:32 Mose aliichukua mifupa ya Yosefu kama Yosefu alivyoagiza kabla ya kufa kwake. Alikuwa amewaapisha rasmi Waisraeli akisema, “Mungu atakapowajia kuwatoa nchini humu, ni lazima mwichukue mifupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi.”
20Basi, Waisraeli waliondoka Sukothi, wakapiga kambi huko Ethamu, ukingoni mwa jangwa. 21Mchana Mwenyezi-Mungu aliwatangulia katika mnara wa wingu kuwaonesha njia, na usiku aliwatangulia katika mnara wa moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana na usiku. 22Taz Hek 10:17-18; 18:3 Mnara wa wingu wakati wa mchana, na mnara wa moto wakati wa usiku, kamwe haikukosekana kuwatangulia Waisraeli.

Kutoka13;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: