Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 6 February 2017

Kikombe Cha Asubuhu;Mwanzo 13...

Shalom,Habari za Asubuhi,Mmeamkaje,Wapendwa/Waungwana?
Siku/wiki Nyingine tena kwa Neema/Rehema za Mungu tumebarikiwa kuiona leo hii..
Tunamshukuru sana Mungu kwa Neema hii,Tuanze wiki hii vyema kwa kumrudishia Mungu Utukufu na Sifa yeye
Astahiliye yote,Mungu wetu aliyeumba Mbingu na Nchi, Yeye ni kimbilio la wote,Yeye akatubariki kuingia/Kutoka kwetu
kwenye Vyombo vya usafiri,Akabariki Kazi zetu,Biashara,Akawaguse na kuwaongoza wanafunzi katika masomo yao, Wapate kukumbuka na kuelewa wanayofundishwa.
Akawaponye Wagonjwa walio Mahospitalini/Majumbani,Wenye Shida/Tabu,Wanaopitia Magumu/Majaribu wamgeukie Mungu na kuomba pasipo kikomo yeye anatosha..
Akawafariji wafiwa,Akawaguse Yatima na Wajane...Wafungwa walio Magerezani pasipo na hatia baba akawaguse, Waliofungwa kwa shida mbalimbali za kidunia,Shetani na minyororo yoyote ya nguvu za Giza Baba ukawafungue na Wakapate Uponyaji..
Tumshukuru Mungu na Kumtukuza,Kuomba na Kuamini yeye ni mwingi wa Huruma na Uponyaji..
Anza na Mungu naye hatokuacha....!!!!
Mungu awabariki Sana.



Abramu na Loti wanatengana

1Abramu akarudi kutoka Misri, akaingia upande wa Negebu. Alikuwa na mkewe na mali yake yote pamoja na Loti. 2Wakati huo, Abramu alikuwa ametajirika sana. Alikuwa na mifugo, fedha na dhahabu. 3Akaendelea kusafiri toka eneo la Negebu hadi Betheli. Alifika mahali alipokuwa amepiga kambi ya hema hapo awali, kati ya Betheli na Ai, 4ambapo alikuwa amejenga madhabahu. Hapo Abramu akamwomba Mwenyezi-Mungu kwa jina lake. 5Kadhalika, Loti, ambaye alifuatana na Abramu, alikuwa na kondoo, mifugo na hema. 6Idadi ya mifugo yao ilikuwa kubwa mno hata nchi ile haikuweza kuwatosha Abramu na Loti kuishi pamoja. 7Basi, kukazuka ugomvi kati ya wachungaji wa Abramu na wachungaji wa Loti. Wakati huo, Wakanaani na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa nchi hiyo.
8Basi, Abramu akamwambia Loti, “Kusiwe na mafarakano kati yetu wala kati ya wachungaji wako na wachungaji wangu, kwa sababu sisi ni jamaa moja. 9Tazama nchi hii yote mbele yako. Na tutengane. Ukienda kushoto, mimi nitakwenda kulia; ukienda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
10Loti akatazama, akaliona bonde la mto Yordani, akaona kuwa lina maji ya kutosha kila mahali, kama bustani ya Mwenyezi-Mungu na kama nchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa kabla Mwenyezi-Mungu hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora). 11Kwa hiyo, Loti akajichagulia bonde lote la mto Yordani, akaelekea mashariki, na hivyo wakatengana. 12Abramu akabaki nchini Kanaani na Loti akakaa kati ya miji iliyokuwa bondeni, akahamishia kambi yake Sodoma. 13Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda dhambi wakuu dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

Abramu anaoneshwa nchi

14Baada ya Loti kujitenga na Abramu, Mwenyezi-Mungu akamwambia Abramu, “Angalia toka hapo ulipo utazame pande zote: Kaskazini, Kusini, Mashariki na Magharibi. 15Nchi hii yote unayoiona nitakupa wewe na wazawa wako iwe yenu milele. 16Wazawa wako nitawafanya wawe wengi wasiohesabika, kama vile mavumbi ya nchi yasivyoweza kuhesabika! 17Basi, inuka uitembelee nchi hii katika mapana na marefu, kwani nitakupa wewe.” 18Kwa hiyo, Abramu akangoa hema, akaenda kukaa karibu na mialoni ya Mamre kule Hebroni; huko akamjengea Mwenyezi-Mungu madhabahu.
Mwanzo 13;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili Mbarikiwe.

No comments: