Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 9 February 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo16...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu ni mwema na Muaminifu..
Tunamshukuru kwa kutuamsha tena siku hii tukiwa wenye afya na kuendelea na maisha ya kila siku ya Duni hii yenye mambo meengi,
Akatuongoze katika kazi zetu,Biashara, Masomo,akavibariki vyombo vyote vya usafiri,tutembeapo,Tuingiapo/Tutokapo baba akawe nasi daima...
Akawaguse na Kuwaponya Wagonjwa,Wanaopitia Magumu/Majaribu, Shida/Tabu zozote Mungu yu pamoja nanyi msiache kumkabidhi yote mnayopitia yeye ni mkombozi wa yote..
Mungu wetu ukawaongoze watoto wetu shuleni wakapate kukumbuka na kuelewa wanayofundishwa,
Ukawalinde na kuwavusha salama katika ujana wao, wakakujue Mungu katika ujana wao mpaka mwisho,Ukawaokoe katika vishawishi vyote vya dunia hii yenye mambo mengi na kufuata mkumbo..
wawe na hofu yako na wasikuonee haya watajapo jina lako mahali popote.
Wazazi/Walezi Mungu ukawape hekima na Busara katika maamuzi na malezi yao.
Tunakwenda kinyume na Mwovu, Nguvu za Giza na vifungo vyote vya shetani.
Tunajiachilia kwako Baba Wambinguni na ukatusamehe pale tulipokosea kwa makusudi/kujua au kutojua..Ukatupe kunena yaliyo yako Mfalme wa Amani uendelee kutawala katika maisha yetu.
Amina..!!!
Mungu awabariki.


Sarai na Hagari
1Basi, Sarai, mkewe Abramu, alikuwa bado hajamzalia mumewe mtoto. Lakini alikuwa na mjakazi aliyeitwa Hagari, kutoka Misri. 2Basi, Sarai akamwambia Abramu, “Unajua kuwa Mwenyezi-Mungu hajanijalia kupata watoto. Mchukue Hagari mjakazi wangu; huenda nikapata watoto kwake.” Abramu akakubali shauri la Sarai.
3Kisha, Sarai akampa Abramu Hagari, mjakazi wake ambaye alikuwa Mmisri, awe mke wake. Haya yalitokea baada ya Abramu kukaa katika nchi ya Kanaani kwa muda wa miaka kumi. 4Abramu akamchukua Hagari, naye Hagari akapata mimba. Lakini mara tu alipoona amepata mimba, Hagari akaanza kumdharau bimkubwa wake. 5Sarai akamwambia Abramu, “Wewe utawajibika kwa ubaya ninaotendewa. Mimi nilikupa mjakazi wangu, lakini alipopata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake! Mwenyezi-Mungu na ahukumu kati yako na mimi!” 6Lakini Abramu akamwambia Sarai, “Mjakazi wako yuko chini ya mamlaka yako; mfanyie upendavyo.” Basi, Sarai akamtesa Hagari mpaka akatoroka.
Ishmaeli anazaliwa
7Malaika wa Mwenyezi-Mungu akamkuta Hagari penye chemchemi ya maji jangwani, chemchemi iliyoko njiani kuelekea Shuri. 8Malaika akamwuliza, “Hagari, mjakazi wa Sarai! Unatoka wapi na unakwenda wapi?” Hagari akamjibu, “Namkimbia bimkubwa wangu Sarai.” 9Yule malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Rudi kwa bimkubwa wako Sarai na umtii.” 10Zaidi ya hayo, malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwambia Hagari, “Nitawazidisha wazawa wako hata wasiweze kuhesabika kwa wingi wao.” 11Kisha huyo malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Wewe ni mjamzito na utajifungua mtoto wa kiume; utamwita Ishmaeli, maana Mwenyezi-Mungu amesikia mateso yako. 12Ishmaeli ataishi kama pundamwitu; atakuwa adui wa kila mtu na kila mtu atakuwa adui yake. Ataishi akiwa adui wa jamaa yake.” 13Basi, Hagari akampa jina Mwenyezi-Mungu aliyezungumza naye huko, “Wewe ni Mungu Aonaye” kwa maana alifikiri, “Kweli hapa nimemwona yeye anionaye!” 14Ndiyo maana kile kisima chaitwa Beer-lahai-roi. Kisima hiki kipo kati ya Kadeshi na Beredi.
15Hagari akamzalia Abramu mtoto wa kiume. Abramu akamwita mtoto huyo Ishmaeli. 16Abramu alikuwa na umri wa miaka 86 wakati Hagari alipomzaa Ishmaeli.
Mwanzo16;1-16
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: